Kwanini DR Congo inataka vikosi vya Afrika Mashariki kuondoka

Maelezo ya picha,

Vikosi hivyo vinajumuisha wanajeshi kutoka Kenya, Burundi, Sudan Kusini na Uganda.

  • Author, Wafula & Kenneth Mungai
  • Nafasi, BBC News, Nairobi

Baada ya kuhudumu kwa miezi 11 tu, kikosi cha Afrika Mashariki kilichoundwa ili kukabiliana na ghasia za wanamgambo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kimeamriwa kuondoka.

Serikali ya Congo ilisema haitaongeza muda wa Jeshi la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) baada ya miezi kadhaa ya Kinshasa kulalamikia kutofanya kazi kwa vikosi hivyo.

Uamuzi wa kutoongeza muda wa wanajeshi hao unakuja huku ghasia kati ya kundi la waasi la M23 na wanamgambo wanaoiunga mkono serikali zikizuka katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa mara nyingine tena.

Je, jukumu la kikosi cha kikanda lilikuwa lipi?

Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) – muungano wa nchi saba – ilituma wanajeshi wake DR Congo mwaka jana baada ya mapigano kuzuka upya kati ya majeshi ya serikali na waasi wa kundi la M23. Kikosi hicho kilikubaliwa muda mfupi baada ya DR Congo kujiunga na Jumuiya hiyo.

Crédit: Lien source

Les commentaires sont fermés.